Mufungwa wa tatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai : Mathieu
Press Release
Mufungwa wa tatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai : Mathieu
ICC-CPI-20080207-PR284
La Haye, siku 7 mwezi ya pili 2008
ICC-CPI-20080207-PR284-SWC
Hali
: Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoAfere :
Prokirere c . Mathieu Ngudjolo ChuiMathieu Ngudjolo Chui, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, anazaniwa kuwa
kiongozi wa zamani wa Front des nationalistes et intégrationnistes (FNI) na kolonele wa jeshi
ya taifa ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC), alikamatiwa jana na
bakubwa ba serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na akapaniwa ku Mahakama ya
Kimataifa ya Jinai. Atafika leo ku munyoro ya Mahakama pale La Haye. Mathieu Ngudjolo
Chui anapashwa kusamba juu ya jinai dhidi ya ubinadamu na jinai za vitani zenye kutayiwa na
ibara 7 na 8 za Mkataba, zenye zilifanyika mu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo tangu mwezi
ya saba 2002.
Siku 6 mwezi ya saba 2007, kisha kujifunza ombi na ushahidi zenye Prokirere alileta, Chumba
cha utangulizi I kilitoa manda ya kukamata
Mathieu Ngudjolo Chui yenye ilikuwa na mhuriya siri. Ile mhuri ya siri ilitoshewa siku 7 mwezi ya pili 2008.
Siku yenye Mathieu Ngudjolo Chui atapita turu ya kwanza mbele ya tribinale itajulishwa
nyuma.
Maneno banamuchongea
Chumba cha utangulizi I kiliona kama kuko sababu za kutosha za kusadiki kama, sawa vile
komanda mkubwa zaidi wa FNI, Mathieu Ngudjolo Chui alikuwa na kazi ya lazima mu
kutayarisha na kushambulia bila kuchagua, kijiji ya Bogoro pale Ituri, siku 24 mwezi ya pili
2003 ao karibu ile siku.
Chumba cha utangulizi kiliona tena kama kuko sababu za kutosha za kusadiki kama,
wakatina kisha shambulizi ya kijiji ya Bogoro yenye iliwinda sanasana basivile ba kabila ya
bahema, na yenye ilifanyika na msaada kabisa ya batoto ba miaka chini ya 15, hizi
maenfraksyo zilifanyika : mauaji ya basivile karibu 200, matendo ya kuumiza sana ku
mwili basivile; kufunga, kutisha na silaha na kufungia basivile mu chumba yenye
inayala maiti; uporaji; kufanya banamuke na batoto banamuke mingi kuwa batumwa
ba kingono.
Tena Chumba cha utangulizi kiliona kama kuko sababu za kutosha za kusadiki kama Mathieu
Ngudjolo Chui na bakomanda bengine bakubwa ba kisoda ba FNI na ba Force de résistance
patriotique en Ituri (FRPI) balisikilizana juu ya mpango ya kushambulia kijiji ya Bogoro, na
kama maenfraksyo zenye zilifanyika ile wakati na kisha ile shambulizi zilikuwa ndani ya
mpango ya pamoja wala zilikuwa, tuseme, matokeo yenye ingeliwezekana na yenye iliitikiwa
ya kutumia ile mupango ya pamoja.
Kufuatana na Chumba, kuko tena sababu za kutosha za kusadiki kama kushambulia Bogoro
ilifanyika mu hali ya vita kule Ituri na kama ilifanyiwa na FNI na FRPI, kati ya mwezi ya
kwanza na ya tatu 2003, mu hali ya shambulizi ya kupangwa na ya mkubwa yenye iliwinda
basivile ba mu mafasi zimoya zimoya za Ituri, sanasana ba kabila ya bahema.
Mashtaka
Ivi njo manda ya kukamata Mathieu Ngudjolo Chui inataya mashtaka kenda yenye
kumubebesha muzigo ya jinai kufuatana na mistari a) wala b) ya ibara 25-3 ya Mkataba wa
Roma :
•
mashtaka tatu ya jinai dhidi ya ubinadamu : mauaji (ibara 7-1-a), matendo yakinyama (ibara 7-1-k) na utumwa wa kingono (ibara 7-1-g)
•
mashtaka sita ya jinai za vitani : mauaji ya kukusudia (ibara 8-2-a-i wala 8-2-c-i),kutendea batu kinyama (ibara 8-2-a-ii) wala matendo ya kikatili (ibara 8-2-c-i),
kuingiza kabisa batoto ba miaka chini ya kumi na tano mu mapigano
(ibara 8-2-b-xxvi wala 8-2-e-vii), utumwa wa kingono (ibara 8-2-b-xxii wala 8-2-e-vi),
kushambulia ku makusudi basivile juu ya hali yabo wala basivile benye habako pale
pale mu mapigano (ibara 8-2-b-i wala 8-2-e-i), na
uporaji ya muji wala mungini,atakama imeshambuliwa
(ibara 8-2-b-xvi wala 8-2-e-v).Masemi ya Grefye
Bruno Cathala, Grefye wa CPI, anafurahi kuona moja wa Nchi zinazounda Mahakama
inatimiza uamuzi ya Mahakama. «Bakubwa ba serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,
bameongeza tena kutumika sana pamoya na Mahakama mu kuheshimia Mkataba na kutimiza
uamuzi ya sheria wakati abo peke balikamata Mathieu Ngudjolo Chui na kumupana ku CPI »,
alisema ivi.
Ukumbusho ya hali ya maneno
Mathieu Ngudjolo Chui njo mutu wa tatu kufungwa na CPI. Siku 17 mwezi ya kumi 2007,
Germain Katanga, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mwenye kuzaniwa kuwa
komanda wa FRPI alipaniwaka ku Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na bakubwa ba serikali ya
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na akapelekewa ku makao makuu ya hii Mahakama.
Anashtakiwa kuwa moya wa benye balifanya maenfraksyo za kabambi zenye zinaweza kuwa
zilifanyika wakati FNI na FRPI zilishambuliaka kijiji ya Bogoro, siku 24 mwezi ya pili 2003 wala
karibu ile siku.
Siku 17 mwezi ya tatu 2006, Thomas Lubanga Dyilo, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo, mwenye kuzaniwa kuwa njo aliundaka na kuongoza Union des patriotes congolais
(UPC), alipelekewaka ku Mahakama.
Prokirere wa Mahakama alianzaka kufanya ankete mu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mu
mwezi ya sita 2004, kisha serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutuma ku Mahakama
hali ya mu Kongo. Hali mu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni moya mu hali ine zenye Biro
ya Prokirere iko inafanya ndani maankete izi siku.
Zingine tatu ni : hali ya Uganda mwenye manda ine za kukamata bakubwa ba Armée de
résistance du Seigneur zilitolewaka siku 8 mwezi ya saba 2005; hali ya Darfour (Soudan)
mwenye manda za kukamata Ahmad Muhammad Harun,
Ministre d’État wa zamani wamambo ya ndani mwenye leo ni
Ministre d’État wa mambo ya kibinadamu mu serikali yaSoudan, na Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman (alias « Ali Kushayb »), kiongozi wa
wanamgambo/Janjaouid zilitolewaka siku 27 mwezi ya ine 2007; na hali mu Jamhuri ya Afrika
ya Kati kwenye ankete iko inafanyika.
Habari za lazima
Mukutano na bapasha habari
Makamu wa Prokirere, Fatou Bensouda, na mshauri mkuu wa kisheria wa biro ya Grefyé,
Phakiso Mochochoko, batafanya mukutano na bapasha habari ku makao makuu ya CPI pale La
Haye, siku ya ine tarehe 7 mwezi ya pili na saa kenda za mchana.
Bapasha habari habalazimishwe kusema kama batakuwa pale.
Batu banaweza kufuata mukutano na bapasha habari ku mtandao ya Internet ya Mahakama,
mu Kifaransa na Kiingereza :
Kiingereza :
http://livestream.xs4all.nl/icc1.asxKifaransa :
http://livestream.xs4all.nl/icc2.asxHabari za kifundi zenye kuangalia utangazaji kupitia satelite zitapaniwa nyuma.
Juu ya habari zaidi, ni muzuri kuongea na Bibi Sonia Robla, mkuu wa Tawi la habari na hifadhi
ya hati. Telefone : +31 (0)70 515-8089 wala telefone ya kumukono +31 (0)6 46 44 87 26; e-mail :
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo : Paul Madidi, afisa wa habari na kuelimisha umma
uwandani. Telefone : +243 99 801 1403 wala e-mail : [email protected]