Communiqué de presse: 7 février 2008

Mufungwa wa tatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai : Mathieu

ICC-CPI-20080207-PR284

Press Release


Mufungwa wa tatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai : Mathieu

ICC-CPI-20080207-PR284

La Haye, siku 7 mwezi ya pili 2008

ICC-CPI-20080207-PR284-SWC

Hali

: Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Afere :

Prokirere c . Mathieu Ngudjolo Chui

Mathieu Ngudjolo Chui, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, anazaniwa kuwa

kiongozi wa zamani wa Front des nationalistes et intégrationnistes (FNI) na kolonele wa jeshi

ya taifa ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC), alikamatiwa jana na

bakubwa ba serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na akapaniwa ku Mahakama ya

Kimataifa ya Jinai. Atafika leo ku munyoro ya Mahakama pale La Haye. Mathieu Ngudjolo

Chui anapashwa kusamba juu ya jinai dhidi ya ubinadamu na jinai za vitani zenye kutayiwa na

ibara 7 na 8 za Mkataba, zenye zilifanyika mu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo tangu mwezi

ya saba 2002.

Siku 6 mwezi ya saba 2007, kisha kujifunza ombi na ushahidi zenye Prokirere alileta, Chumba

cha utangulizi I kilitoa manda ya kukamata

Mathieu Ngudjolo Chui yenye ilikuwa na mhuri

ya siri. Ile mhuri ya siri ilitoshewa siku 7 mwezi ya pili 2008.

Siku yenye Mathieu Ngudjolo Chui atapita turu ya kwanza mbele ya tribinale itajulishwa

nyuma.

Maneno banamuchongea

Chumba cha utangulizi I kiliona kama kuko sababu za kutosha za kusadiki kama, sawa vile

komanda mkubwa zaidi wa FNI, Mathieu Ngudjolo Chui alikuwa na kazi ya lazima mu

kutayarisha na kushambulia bila kuchagua, kijiji ya Bogoro pale Ituri, siku 24 mwezi ya pili

2003 ao karibu ile siku.

Chumba cha utangulizi kiliona tena kama kuko sababu za kutosha za kusadiki kama,

wakati

na kisha shambulizi ya kijiji ya Bogoro yenye iliwinda sanasana basivile ba kabila ya

bahema, na yenye ilifanyika na msaada kabisa ya batoto ba miaka chini ya 15, hizi

maenfraksyo zilifanyika : mauaji ya basivile karibu 200, matendo ya kuumiza sana ku

mwili basivile; kufunga, kutisha na silaha na kufungia basivile mu chumba yenye

inayala maiti; uporaji; kufanya banamuke na batoto banamuke mingi kuwa batumwa

ba kingono.

Tena Chumba cha utangulizi kiliona kama kuko sababu za kutosha za kusadiki kama Mathieu

Ngudjolo Chui na bakomanda bengine bakubwa ba kisoda ba FNI na ba Force de résistance

patriotique en Ituri (FRPI) balisikilizana juu ya mpango ya kushambulia kijiji ya Bogoro, na

kama maenfraksyo zenye zilifanyika ile wakati na kisha ile shambulizi zilikuwa ndani ya

mpango ya pamoja wala zilikuwa, tuseme, matokeo yenye ingeliwezekana na yenye iliitikiwa

ya kutumia ile mupango ya pamoja.

Kufuatana na Chumba, kuko tena sababu za kutosha za kusadiki kama kushambulia Bogoro

ilifanyika mu hali ya vita kule Ituri na kama ilifanyiwa na FNI na FRPI, kati ya mwezi ya

kwanza na ya tatu 2003, mu hali ya shambulizi ya kupangwa na ya mkubwa yenye iliwinda

basivile ba mu mafasi zimoya zimoya za Ituri, sanasana ba kabila ya bahema.

Mashtaka

Ivi njo manda ya kukamata Mathieu Ngudjolo Chui inataya mashtaka kenda yenye

kumubebesha muzigo ya jinai kufuatana na mistari a) wala b) ya ibara 25-3 ya Mkataba wa

Roma :

mashtaka tatu ya jinai dhidi ya ubinadamu : mauaji (ibara 7-1-a), matendo ya

kinyama (ibara 7-1-k) na utumwa wa kingono (ibara 7-1-g)

mashtaka sita ya jinai za vitani : mauaji ya kukusudia (ibara 8-2-a-i wala 8-2-c-i),

kutendea batu kinyama (ibara 8-2-a-ii) wala matendo ya kikatili (ibara 8-2-c-i),

kuingiza kabisa batoto ba miaka chini ya kumi na tano mu mapigano

(ibara 8-2-b-xxvi wala 8-2-e-vii), utumwa wa kingono (ibara 8-2-b-xxii wala 8-2-e-vi),

kushambulia ku makusudi basivile juu ya hali yabo wala basivile benye habako pale

pale mu mapigano (ibara 8-2-b-i wala 8-2-e-i), na

uporaji ya muji wala mungini,

atakama imeshambuliwa

(ibara 8-2-b-xvi wala 8-2-e-v).

Masemi ya Grefye

Bruno Cathala, Grefye wa CPI, anafurahi kuona moja wa Nchi zinazounda Mahakama

inatimiza uamuzi ya Mahakama. «Bakubwa ba serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,

bameongeza tena kutumika sana pamoya na Mahakama mu kuheshimia Mkataba na kutimiza

uamuzi ya sheria wakati abo peke balikamata Mathieu Ngudjolo Chui na kumupana ku CPI »,

alisema ivi.

 

Ukumbusho ya hali ya maneno

Mathieu Ngudjolo Chui njo mutu wa tatu kufungwa na CPI. Siku 17 mwezi ya kumi 2007,

Germain Katanga, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mwenye kuzaniwa kuwa

komanda wa FRPI alipaniwaka ku Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na bakubwa ba serikali ya

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na akapelekewa ku makao makuu ya hii Mahakama.

Anashtakiwa kuwa moya wa benye balifanya maenfraksyo za kabambi zenye zinaweza kuwa

zilifanyika wakati FNI na FRPI zilishambuliaka kijiji ya Bogoro, siku 24 mwezi ya pili 2003 wala

karibu ile siku.

Siku 17 mwezi ya tatu 2006, Thomas Lubanga Dyilo, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya

Kongo, mwenye kuzaniwa kuwa njo aliundaka na kuongoza Union des patriotes congolais

(UPC), alipelekewaka ku Mahakama.

Prokirere wa Mahakama alianzaka kufanya ankete mu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mu

mwezi ya sita 2004, kisha serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutuma ku Mahakama

hali ya mu Kongo. Hali mu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni moya mu hali ine zenye Biro

ya Prokirere iko inafanya ndani maankete izi siku.

Zingine tatu ni : hali ya Uganda mwenye manda ine za kukamata bakubwa ba Armée de

résistance du Seigneur zilitolewaka siku 8 mwezi ya saba 2005; hali ya Darfour (Soudan)

mwenye manda za kukamata Ahmad Muhammad Harun,

Ministre d’État wa zamani wa

mambo ya ndani mwenye leo ni

Ministre d’État wa mambo ya kibinadamu mu serikali ya

Soudan, na Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman (alias « Ali Kushayb »), kiongozi wa

wanamgambo/Janjaouid zilitolewaka siku 27 mwezi ya ine 2007; na hali mu Jamhuri ya Afrika

ya Kati kwenye ankete iko inafanyika.

Habari za lazima

Mukutano na bapasha habari

Makamu wa Prokirere, Fatou Bensouda, na mshauri mkuu wa kisheria wa biro ya Grefyé,

Phakiso Mochochoko, batafanya mukutano na bapasha habari ku makao makuu ya CPI pale La

Haye, siku ya ine tarehe 7 mwezi ya pili na saa kenda za mchana.

Bapasha habari habalazimishwe kusema kama batakuwa pale.

Batu banaweza kufuata mukutano na bapasha habari ku mtandao ya Internet ya Mahakama,

mu Kifaransa na Kiingereza :

Kiingereza :

http://livestream.xs4all.nl/icc1.asx

Kifaransa :

http://livestream.xs4all.nl/icc2.asx

Habari za kifundi zenye kuangalia utangazaji kupitia satelite zitapaniwa nyuma.

 

Juu ya habari zaidi, ni muzuri kuongea na Bibi Sonia Robla, mkuu wa Tawi la habari na hifadhi

ya hati. Telefone : +31 (0)70 515-8089 wala telefone ya kumukono +31 (0)6 46 44 87 26; e-mail :

[email protected]

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo : Paul Madidi, afisa wa habari na kuelimisha umma

uwandani. Telefone : +243 99 801 1403 wala e-mail : [email protected]